» » Faida za kufanya usafi na Hasara za kutokufanya usafi ktk Computer Yako

Kwanza kabisa ninaomba kuanza na utagulizi kama ifuatavyo, tunapo zungumzia usafi ktk Computer tunamaanisha usafi wa aina mbili;
  1. Usafi wa ndani ya Mafaili na Software za Computer (Software and File checkup and maintenance)
  2. Usafi wa vifaa vyote vya ndani na nje ya Computer (Hardware checkup and maintenance)

Ufanyaji usafi ktk Computer yako una faida nyingi sana ikiwemo;
  1. Kuongeza urefu wa maisha ya Computer yako
  2. Kuongeza umahiri wa Computer yako ktk utendaji kazi
  3. Kupunguza gharama za ununuaji vifaa vilivyoharibika kwa kupuuza kufanya usafi
  4. Kuepusha Computer kuzimika ghafla kwa kuzidiwa na uchafu au wadudu
  5. Kufanya Computer iwe na spidi kama ilivyounuliwa mwanzo

Kutokufanya usafi ktk Computer yako kuna hasara zifuatazo;
  1. Inaweza kucrash au kufeli na kuzimika ghafla
  2. Spidi ndogo ktk utendaji kazi
  3. Kukosa umahiri ktk utendaji kazi, yaani haitakuwa na uwezo wa kufanya kazi kwa muda mrefu na itakuwa inachemka na pengine kuzimika baada ya muda mfupi
  4. Gharama kubwa siku ambayo Computer imeharibika sababu itakuwa imeharibu vifaa vingi
  5. Utakuwa umeipunguzia urefu wa maisha yake maana haitadumu hata kwa muda wa miaka miwili

Hivyo basi, usafishaji wa Computer SAHIHI, unafanywa na wanaofahamu tu yaani maexpert wa IT, na kuna mambo mengi sana yanayotakiwa kufanywa, hivyo basi kama na wewe ni miongoni mwao inabidi ufanye haraka kuwaona wataalamu.

About Unknown

Hi there! I am Hung Duy and I am a true enthusiast in the areas of SEO and web design. In my personal life I spend time on photography, mountain climbing, snorkeling and dirt bike riding.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply